Biashara Ni Vita

Sehemu 6

EPISODE 6: Pesa Zinaongea (Capital vs Profit)

Biashara Ni Vita • Aisha Mtamu

Biashara ya Juma, J Classic Wear, ilikuwa sasa inaonekana kabisa imeanza kukua. Kila siku kulikuwa na mauzo. Simu yake ilikuwa busy. Wateja walikuwa wanarudi tena na tena. Lakini ndani yake… Kulikuwa na tatizo moja hatari sana — ambalo hakuliona mapema. Siku moja… Juma alihesabu pesa zake jioni. Alikuwa na zaidi ya Tsh 350,000 mkononi. Alitabasamu. “Hatimaye nimeanza kuona pesa,” alisema. Kesho yake… Akanunua: Simu mpya Viatu vipya Na akatoka kula na marafiki Alijiona amefanikiwa. Lakini hakujua… Pesa zote unazoona sio faida… nyingine ni mtaji wako. Baada ya siku chache… Alitaka kwenda kununua mzigo mpya wa nguo. Alipohesabu pesa… Akashangaa. “Mbona haitoshi?” Moyo wake ulianza kwenda mbio. “Lakini nilikuwa na pesa nyingi…” Alimpigia Khalid haraka. “Bro, sijui nini kinaendelea… pesa imepotea!” Khalid alimuuliza swali moja tu: “Uliwahi kutenganisha faida na mtaji?” Juma alikaa kimya. Hakuwahi kufanya hivyo. Khalid akamwambia: Ukichanganya mtaji na matumizi binafsi, biashara yako itaonekana inakua… lakini inakufa taratibu. Juma alihisi aibu. Lakini pia alijifunza. Khalid alimfundisha mfumo rahisi: 1. Mtaji (Capital) – pesa ya kununua mzigo 2. Faida (Profit) – pesa inayobaki baada ya gharama 3. Matumizi binafsi – pesa ya maisha

NOTE: Usitumie pesa ya biashara kama ATM. Jiwekee mfumo wa kujilipa (salary) ili biashara ikue.

Juma alichukua hatua. Alianza: Kuandika kila mauzo Kuandika kila matumizi Kutenganisha pesa Mwanzoni ilikuwa ngumu… Lakini polepole akaanza kuona tofauti. Baada ya wiki mbili… Aliweza kusema kwa uhakika: “Hii ndio faida yangu halisi.” Na kwa mara ya kwanza… Biashara yake ilianza kuwa chini ya control. Lakini kadri pesa zilivyoanza kuonekana… Kulikuwa na hatari nyingine kubwa zaidi ilianza kumkaribia: Mikopo na madeni. Sio kila pesa inayokuja kwako ni ya kuchukua… nyingine ni mtego. 👉 Episode 7 itakuwa hatari sana 🔥 Tutazungumzia mikopo, madeni na washkaji wanaokukopesha Na jinsi watu wengi wanavyoanguka kwenye biashara

Maoni

Hakuna maoni bado

Profaili

Alama ya uaminifu